PATA HABARI MUHIMU KUTOKA VISIWA VYA ZIWA VICTORIA PAMOJA NA HABARI ZA MICHEZO ZA KIMATAIFA

Jumanne, 30 Julai 2013
LEWANDOWSKI asema ''NITAWEKA UWEZO WANGU WOTE KWA DORTMUND''
Mchezaji aliyekuwa na misukosuko katika kipindi hiki cha usajili Robert Lewandowski wa klabu ya nchini Ujerumani ya Borrusia Dortmund, amesema yuko tayari kucheza kwa kiwango chake chote katika klabu yake hiyo. Mchezaji huyo aliyekuwa ameamua kuihama klabu yake kutimukia klabu ya Bayern Munich, alikutana na vikwazo kibao kutoka kwenye klabu yake na kuishia kushindwa kutimiza lengo lake la kuhama. Baada ya kucheza mchezo wa SUPER CUP, Borrusia Dortmund iliishinda klabu ya Bayern Munich kwa goli 4-2, baada ya mchezo huo, mchezaji huyo raia wa Polandi alisema ameamua kurudisha mapenzi yake kwa Dortmund kwani alikwisha poteza mahusiano ya karibu hata na wachezaji wenzake klabuni humo. '' Niko tayari kushinda mataji mengine zaidi ya hili (super cup) nikiwa na klabu yangu ya Borrusia Dortmund'' alisema mchezaji huyo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni