Jumanne, 23 Julai 2013

PATA HABARI MUHIMU ZA TETESI ZA USAJILI KWENYE LIGI MBALIMBALI HUKO MAJUU
Klabu ya Napoli ya nchini italia, imekubaliana na waliokuwa mabingwa wa ligi ya Uhispania mwaka jana klabu ya Real Madrid, kulipa kiasi cha Yuro milioni 37 ili kumsajili mshambuliaji raia wa Ajentina Gonzalo Higuani. Mchezaji huyo ambaye anasakwa wa udi na uvumba na klabu ya Arsenal, bado hajakubaliana na klabu hiyo kongwe ya Italia. Pamoja na makubaliano hayo kati ya timu mbili hizo, Higuani tayari ameshakubaliana na klabu ya Arsenal kila kitu ikiwamo mshahara wa mchezaji huyo. Higuan ambaye analipwa kiasi cha Yuro 75 elfu kwa wiki katika klabu yake ya sasa, amekubaliana na Arsenal kulipwa kiasi cha Yuro 116,000/= kwa wiki, ikiwa ni msahara wa kuanzia, hata ivyo klabu ya Napoli nayo iko tayari kumlipa mchezaji huyo kiasi hicha cha mshahara. Tatizo linaonekana kutokubaliana kwa malipo ya kumnunua mchezaji huyo kati ya timu ya Arsenal na timu ya Real Madrid. Napoli inasaka mshambuliaji wa kati baada ya kumuuza mchezaji wao Cavani kwa matajiri wa Ufaransa klabu ya P.S.G. Hata ivyo Higuan bado ana mkataba wa miaka 2 na timu yake hiyo.
Klabu ya Arsenal ya jijini London, iko katika wakati mzuri wa kumsajili kiungo mchezeshaji kutoka katika timu ya Atletico Mineiro. Mblazili Bernad ambaye anatajwa kutakwa na vilabu vingi kama Tottenham, Liverpool, Borussia Dortmund pamoja na Shakhtar Donetsk, tayari amekwishakubaliana na klabu ya Arsenal kumlipa mshahara wa paund 50,000/ kwa wikina ada kutoka kwenye klabu yake kiasi cha paund milion 21, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20, ana uwezo wa kucheza kama kiungo mchezeshaji na winga. Timu ya Arsenal imechangwanywa na soko la wachezaji kutokana na jinsi ambavyo linaendelea. WAKATI HUOHUO klabu ya Arsenal inajiandaa kuongeza dau ili kujaribu kuishawishi klabu ya Liverpool kuwauzia mshambuliaji wao hata Luis Suarez, mchezaji huyo ameonyesha kuwa tayari kujiunga na klabu hiyo ya London ili acheze ligi kuu ya mabingwa msimu huu.


                              

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni