Jumanne, 30 Julai 2013

SITAKI KWENDA MAN U, NATAKA KUBAKI BARCA

Kocha David Moyes wa Man U anaonekana kuangukia pua kwa lengo lake la kumsajili kiungo mchezeshaji raia wa Hispania Cesc Fabregas, kiungo huyo alikuwa ndo chagua la kwanza katika dirisha la usajili msimu huu kwa kocha mpya wa Man U. Moyes alikuwa tayari ameshatenga kiasi cha paundi milioni 35 kwa ajili ya ada ya kumsajili kijana huyo. Kitendo cha mchezaji huyu mwenye umri wa miaka 26 kutamka kwamba atasalia kwenye klabu yake bingwa wa ligi mwaka huu. Mchezaji huyo amenukuliwa akiwaambia marafiki zake kwamba watakuwa wote Camp nou msimu ujao na anapenda kuendelea kusakata kabumbu kwenye klabu ya Barcelona msimu huu. Inaonekana kwamba baada ya Moyes kumkosa kiungo huyo, sasa amehamishia nguvu zake kwa kiungo wa zamani wa klabu ya Tottenham aliyeko klabu ya Real Madrid Luka Modric pia ametenga kiasi cha yuro milioni 25 ili kumnasa kiungo aliyekuwa naye kwenye klabu ya Everton mbeligiji Marouane Fellaini ambaye analipwa na klabu yake ya sasa kiasi cha yuro 87,000 kwa wiki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni