Jumanne, 30 Julai 2013

TUWE NA SHUKRANI KWA MOURINHO-CASILLAS

Kapteni wa klabu ya Real Madrid mkongwa Ike Casillas, ameshauri iwepo shukrani kwa aliyekuwa kocha wao Jose Mourinho, mlinda mlango huyo aliyejikuta anapoteza nafasi yake ya kikosi cha kwanza mwishoni mwa msimu uliopita, amesema kocha huyo anayeinoa klabu ya matajiri wa London kwa sasa inabidi apewe heshima yake kwani amefanya makubwa kwa kipindi cha miaka mitatu aliyokaa Santiago Bernabeu. '' Kwa sasa ninafundishwa na kocha mwingine, lakini bado sijaona utofauti wowote'' alitanabaisha mlinda mlango huyo wa timu ya taifa ya Hispania. Miaka mitatu aliyokaa Jose Mourinho ameweza kubeba mataji matatu lakini kuna baadhi ya wadau wa soka wanaobeza kazi aliyoifanya kocha huyo. ''Najua kuwa kuna magolikipa wazuri katika klabu yangu lakini inanibidi niwe na juhudi ili kuwa namba moja'' alisema mkongwe Casillas.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni